Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Ushauri wangu kwa leo, ni Heri kuchagua kunyamaza

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

MITHALI 11:12 Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

MITHALI 17:28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kwamba tunataka kuongea kila wakati, tunataka kujibu kila tunachokisikia, kila tunachokiona tunataka kukisemea kitu.

Kuna wakati tunasikia na kukutana na mambo ambayo kiuhalisia moyo unagoma kabisa kunyamaza, unatamani ujibu, unatamani uwaambie watu yale umefanyiwa, unatamani uelezee vile umeumizwa lakini kumbe si kila jambo linatakiwa kuongelewa.

Si kila ukionacho unatakiwa kukisemea kitu. Si kila usikiacho/uambiwacho ni lazima ujibu.

Si kila ufanyiwacho ni lazima umwambie kila mtu.

MUHUBIRI 3:1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

Ipo nguvu katika kunyamaza

Yapo mambo ambayo tunapaswa kuongea, kusema, lakini yapo mambo ambayo tunapaswa kunyamaza kwa ajili ya usalama wa Roho zetu.

Ni kweli kuna wakati unasemwa sana vibaya, unasingiziwa, unatukanwa nk nk, lakini ni lazima ukumbuke kwamba kuna mazingira ambayo hupaswi kujibizana hata kama umeumia kiasi gani.

Unajua ni kwanini?

Ukisemwa vibaya, ukitukanwa, ukidharauliwa lazima moyo utaghafilika, moyo ukighafilika lazima utakuwa na hasira na ghadhabu.

Ukiwa na hasira katu usitegemee kuwa utajadiliana na mtu kwa hekima.

Ukiongea utaongea katika uwepo wa hasira, ukijibu utajibu kulingana na kiwango cha hasira ulichonacho.

Sasa jiulize majibu yanayotoka kutokana na msukumo wa hasira huwa yanakuwaje?

Mazuri? Ya upole? Ya hekima? Ya unyenyekevu? I am sure jibu ni hapana.

Kama jibu ni hapana that means utaongea vitu vibaya ambavyo ni chukizo kwa MUNGU kwa sababu amesema maneno yetu na yakolee munyu (chumvi).

Sasa badala ya kuongea upumbavu na ukamkosea MUNGU kwanini usichague kunyamaza?

AMOSI 5:3 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya.

Nimekuwa inspired sana na mwanamke Abigaili, ni kweli mumewe alikuwa na makosa, ni kweli alikuwa mlevi, lakini mwanamke huyu alijua ni wakati gani, na mazingira gani alipaswa kuongea na mumewe na alijua aongee nini. Alipomkuta mumewe yupo katika hali ya ulevi, ALINYAMAZA, alijua kuwa huu sio wakati wa kusema jambo lolote.

1 SAMWELI 25:1

Ni vyema sisi pia tukajifunza kusoma mazingira na nyakati na hali za watu zilivyo ili tujue ni wakati gani tujibu, tuongee nini na ni wakati gani tunyamaze

Kilinde kinywa, hakikisha haukiachi kinene mabaya – ZABURI 50:19.

Usipoteze marafiki na kuharibu mahusiano kwa ajili ya kinywa kibovu – MITHALI 11:9.

Ni vyema tukajifunza kujua ni neno gani tukitamka kwa wakati/hali/mazingira gani litakubaliwa –MITHALI 10:32.

ZABURI 19:14 – Bwana na akafanye maneno yetu yakapate kibali mbele zake MUNGU na mbele za wanadamu pia.

1SAMWELI 25:36

Umeumizwa, umekwazwa, umetukanwa, umedharauliwa, KATIKA MAZINGIRA YA HASIRA NA GHADHABU JITAHIDI KUNYAMAZA.

Ni kweli moyo na akili na hisia vinakusukuma kujibu, kubisha nk nk, lakini elewa impact za kujibizana ukiwa na hasira na hizo ni bora ukae kimya.

*"AKUSHINDAE KUONGEA, MSHINDE KUNYAMAZA
"Uwe na siku njema!

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 51

Please log in or register to comment or reply.
👥 Alex Nyamweya Guest Jun 27, 2024
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Guest Guest Oct 6, 2025
asante kwa mafundisho mazuri
👥 Alice Mwikali Guest Jun 5, 2024
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Lydia Wanyama Guest Apr 23, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Joseph Mallya Guest Dec 6, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Joseph Kitine Guest Oct 18, 2023
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Esther Cheruiyot Guest Sep 19, 2023
Endelea kuwa na imani!
👥 Rose Waithera Guest Apr 22, 2023
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Joy Wacera Guest Apr 7, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Linda Karimi Guest Mar 11, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Nora Kidata Guest Aug 1, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Paul Ndomba Guest Feb 2, 2022
Baraka kwako na familia yako.
👥 Elizabeth Mtei Guest Aug 14, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Henry Sokoine Guest Aug 16, 2020
Dumu katika Bwana.
👥 Thomas Mwakalindile Guest Jul 17, 2020
Sifa kwa Bwana!
👥 Rose Mwinuka Guest May 28, 2020
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Fredrick Mutiso Guest May 14, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Ann Wambui Guest Apr 3, 2020
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Henry Sokoine Guest Dec 7, 2019
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Josephine Nduta Guest Sep 16, 2019
Rehema zake hudumu milele
👥 Alice Jebet Guest Jun 7, 2019
Imani inaweza kusogeza milima
👥 George Tenga Guest May 6, 2019
Mwamini katika mpango wake.
👥 Lydia Mutheu Guest Mar 28, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Margaret Anyango Guest Jan 28, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Alice Jebet Guest Sep 10, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Kevin Maina Guest Aug 2, 2018
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Grace Majaliwa Guest Jul 7, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
👥 Stephen Kikwete Guest May 14, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Grace Mushi Guest Mar 21, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Daniel Obura Guest Feb 2, 2018
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Mercy Atieno Guest Jul 13, 2017
Neema na amani iwe nawe.
👥 Raphael Okoth Guest Jul 12, 2017
Rehema hushinda hukumu
👥 Joseph Mallya Guest May 12, 2017
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Lydia Mahiga Guest May 9, 2017
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Joyce Aoko Guest Mar 27, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Andrew Mchome Guest Dec 29, 2016
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Kevin Maina Guest Oct 16, 2016
Nakuombea 🙏
👥 Dorothy Nkya Guest Jun 17, 2016
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Josephine Nduta Guest May 18, 2016
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Alex Nyamweya Guest May 12, 2016
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Margaret Anyango Guest Apr 27, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Catherine Mkumbo Guest Apr 17, 2016
Mungu akubariki!
👥 George Wanjala Guest Mar 6, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Lydia Mzindakaya Guest Feb 5, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Anna Malela Guest Oct 15, 2015
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Mary Kendi Guest Jul 31, 2015
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Edwin Ndambuki Guest Jul 13, 2015
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Joyce Aoko Guest Jul 2, 2015
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Benjamin Masanja Guest May 30, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Grace Njuguna Guest May 5, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 James Kimani Guest Apr 24, 2015
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About