Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, JUNI 04, 2023: SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU - Jumapili baada ya Pentekoste

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

MWANZO:

Asifiwe Mungu Baba na Mwana na Roho Mtakatifu; kwasababu ametufanyizia huruma yake.

SOMO 1

Kut. 34 : 4-6, 8-9

Musa aliinuka na mapema asubuhi, naye akakwea katika mlima wa Sinai, kama Bwana alivyomwamuru, akazichukua hizo mbao mbili za mawe mkononi mwake.

Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana. Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; Musa akafanya haraka, akainamisha kichwa chake hata nchi, akasujudu. Akasema, Ikiwa sasa nimepata neema mbele zako, Bwana, nakuomba, Bwana, uende kati yetu maana ni watu wenye shingo ngumu; ukasamehe uovu wetu na dhambi yetu, ukatutwae tuwe urithi wako.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu

WIMBO WA KATIKATI

Dan. 3:52-56. (K) 52

(K) Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.

Umehimidiwa, Ee Bwana, Mungu wa baba zetu:

Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.

Limehimidiwa jina lako takatifu, tukufu;

Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. (K)

Umehimidiwa katika hekalu la fahari yako takatifu;

Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.

Umehimidiwa juu ya kiti cha ufalme wako;

Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. (K)

Umehimidiwa utazamaye vilindi, uketiye juu ya makerubi;

Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.

Umehimidiwa katika anga la mbinguni

Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele. (K)

SOMO 2

2 Kor. 13 :11-14

Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfariji- ke, nieni mamoja, mkae katika amani; na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi. Sali- mianeni kwa busu takatifu. Watakatifu wote wawasalimu. Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu. na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

SHANG1LIO

Ufu. 1 :8

Aleluya, Aleluya,

Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, Mungu ambaye yupo, aliyekuwako, na atakayekuja.

Aleluya.

INJILI

Yn. 3:16-18

Yesu alimwambia Nikodemu: Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhu- kumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Esther Cheruiyot Guest Jul 3, 2024
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Michael Onyango Guest May 23, 2024
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ James Mduma Guest May 6, 2024
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Janet Mbithe Guest May 4, 2024
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Ruth Mtangi Guest Mar 17, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Ruth Mtangi Guest Feb 29, 2024
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Fredrick Mutiso Guest Jan 20, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Monica Nyalandu Guest Jan 16, 2024
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Simon Kiprono Guest Oct 22, 2023
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Josephine Nekesa Guest Oct 14, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Alice Mrema Guest Aug 11, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Grace Njuguna Guest Jan 24, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Fredrick Mutiso Guest Oct 24, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Peter Otieno Guest Jul 2, 2022
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Malima Guest Jun 20, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Nora Kidata Guest Feb 25, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Malima Guest Feb 22, 2022
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mahiga Guest Dec 7, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Mary Kidata Guest Oct 27, 2021
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Betty Cheruiyot Guest Jul 6, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Joseph Mallya Guest Mar 10, 2021
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Wilson Ombati Guest Dec 25, 2020
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Alice Jebet Guest Dec 14, 2020
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Peter Mwambui Guest Nov 3, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Grace Minja Guest Aug 14, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Nicholas Wanjohi Guest Aug 11, 2020
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Josephine Nduta Guest Jul 11, 2020
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Catherine Mkumbo Guest Apr 26, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Mary Mrope Guest Feb 7, 2020
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Faith Kariuki Guest Jan 2, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Diana Mumbua Guest Dec 30, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Peter Mwambui Guest Aug 5, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Betty Akinyi Guest Apr 14, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Charles Wafula Guest Apr 5, 2019
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Janet Sumaye Guest Sep 22, 2018
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mahiga Guest May 15, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ George Mallya Guest Mar 21, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Peter Otieno Guest Dec 21, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Malima Guest Dec 12, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Francis Mtangi Guest Nov 7, 2017
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Philip Nyaga Guest Aug 31, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Bernard Oduor Guest May 13, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Josephine Nekesa Guest Apr 8, 2017
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Jackson Makori Guest Apr 6, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Edward Lowassa Guest Jun 19, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Peter Mbise Guest Dec 9, 2015
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Joyce Aoko Guest Nov 10, 2015
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Esther Nyambura Guest Oct 30, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Peter Mugendi Guest Jul 3, 2015
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Anna Mchome Guest Apr 8, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About