Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, MARCHI 16, 2022: JUMATANO, JUMA LA 2 LA KWARESIMA

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Yer. 18-18-20

Waliposema, Njoni na tufanye mashauri juu ya Yeremia; maana sheria haitampotea kuhani, wala shauri halitampotea mwenye hekima, wala neno halitampotea nabii. Njoni, na tumpige kwa ndimi zetu, wala tusiyaangalie maneno yake yoyote.

Niangalie, Ee Bwana, ukasikilize sauti ya wanaoshindana nami. Je! Mabaya yalipwe badala ya mema? Maana wameichimbia nafsi yangu shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele zako, ili nisema mema kwa ajili yao, nikaigeuze ghadhabu yako isiwapate.

Neno la Bwanaโ€ฆ Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 31:4-5, 13-15 (K) 16

(K) Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako, Ee Bwana.

Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri,

Maana Wewe ndiwe ngome yangu.

Mikononi mwako naiweka roho yangu;

Umenikomboa, Ee Bwana, Mungu wa kweli. (K)

Maana nimesikia masingizio ya wengi;

Hofu ziko pande zote.

Waliposhauriana juu yangu,

Walifanya hila wauondoe uhai wangu. (K)

Lakini mimi nakutumaini Wewe, Bwana,

Nimesema, Wewe ndiwe Mungu wangu.

Nyakati zangu zimo mikononi mwako;

Uniponye na adui zangu, nao wanaonifuatia. (K)

SHANGILIO

Lk. 8:15

Heri wale walishikao neno la Mungu katika moyo wao mwema na unyofu, na wazaao matunda katika uvumilivu.

INJILI

Mt. 20:17-28

Yesu alipokuwa akipanda kwenda Yerusalemu aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani; na njiani akawaambia, Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi nao watamhukumu afe; kisha watampeleka kwa Mataifa wapate kumdhihaki, na kumpiga mijeledi na kumsulibisha; na siku ya tatu atafufuka.

Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno. Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako. Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza. Akawaambia, Hakika mtakinywa kikombe change; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.

Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili. Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha. Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu yeyote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu; na mtu yeyote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu; kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Ann Wambui Guest Jun 17, 2024
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Esther Cheruiyot Guest Apr 22, 2024
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ James Kawawa Guest Dec 8, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ James Malima Guest Sep 5, 2023
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Agnes Sumaye Guest Jun 26, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Linda Karimi Guest Feb 19, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Nicholas Wanjohi Guest Oct 12, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Andrew Odhiambo Guest Aug 1, 2022
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ John Lissu Guest May 27, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Mwakalindile Guest Apr 2, 2022
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Charles Mboje Guest Jan 28, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Rose Lowassa Guest Jan 14, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Edith Cherotich Guest Nov 16, 2021
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Janet Mwikali Guest Nov 9, 2021
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Chris Okello Guest Nov 8, 2021
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Mary Sokoine Guest Oct 25, 2021
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Grace Mligo Guest Sep 19, 2021
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Alice Mwikali Guest Sep 1, 2021
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Janet Mwikali Guest Jun 2, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Grace Majaliwa Guest Apr 19, 2021
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Chris Okello Guest Jan 31, 2021
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrema Guest Jan 12, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Robert Ndunguru Guest Dec 6, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Charles Wafula Guest Dec 3, 2020
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Brian Karanja Guest Oct 1, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Sharon Kibiru Guest May 2, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Margaret Mahiga Guest Mar 23, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Victor Sokoine Guest Feb 18, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Anthony Kariuki Guest Jan 20, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Bernard Oduor Guest Jan 19, 2020
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Patrick Akech Guest Oct 1, 2019
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Nancy Kabura Guest May 2, 2019
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Irene Makena Guest Feb 26, 2019
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Edwin Ndambuki Guest Feb 5, 2019
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Sarah Mbise Guest Aug 8, 2018
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Grace Mushi Guest Mar 27, 2018
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mahiga Guest Mar 14, 2018
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Peter Mbise Guest Mar 4, 2018
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Nora Lowassa Guest Jan 1, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Lydia Wanyama Guest Jun 27, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Anthony Kariuki Guest Dec 17, 2016
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mushi Guest Jul 25, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Janet Mwikali Guest Apr 19, 2016
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Paul Ndomba Guest Jan 2, 2016
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Stephen Malecela Guest Oct 20, 2015
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Aug 9, 2015
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Francis Njeru Guest Aug 4, 2015
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Nancy Komba Guest Jul 28, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kitine Guest Jun 8, 2015
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Alice Jebet Guest Apr 25, 2015
Sifa kwa Bwana!

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About